Sunday, May 30, 2010

Dalili za kupatwa na jinni

Dalili za kupatwa na Jinni

Dalili unapokuwa macho(ukiwa hujalala)
1.Kujisikia unachukia kufanya Ibada , kuchukia kufanya Dhikr
Angalia Quraan 43:36-37
2Kufanya makosa makosa katika kauli(maneno) , kutembea kwa kuangukaanguka2:275
3.Kuanguka kama kifafa bila ya kuwa na ugonjwa wa kuanguka kifafa nah ii ni moja katika dalili za kupatwa na jinni ima la kutupiwa au jinni la upepo mbaya(pepo mbaya)
4.Miguu kuwa haina nguvu(kupalalaizi) bila sababu maalum ya kitabibu
5 Kuwa na hasira bila sababu , au kulia bila sababu ya msingi
6.Kukaa chooni kwa muda mrefu na kuongea pekee yako na kujijibu
7Kuumwa kichwa mara kwa mara , na kichwa hakitulii hata ukinywa vidonge
8.Kwa upande wa wanawake kutokwa damu bila mpango maalum wa siku zao, angalizo katika hili kuna wanawake wenye Anemia wamuone daktari kwanza.
9.Kutokupata watoto, ingawa mume na mke wote ni wazima na wana uwezo wa kuzaa
Kuna dalili nyingi mno ila hizi ni katika hizo dalili

Dalili unapokuwa usingizini
1.Kupata ndoto za kutisha , ambazo zinakufanya kuona viumbe vya ajabu na vya kutisha, kujiona unaanguka toka ghorofani au unaanguka katika shimo, kuona nyoka usingizini.Kuota kuingiliana kimwili na mtu usiyemfahamu na kumuona mtu anakutisha usingizini

2.Kuwa msahaulifu , kuwa na wasiwasi, na kuwa muoga (unakuwa mwoga)wakati wa kuamka
3.Kuongea kwa sauti kubwa(kupayuka) ukiwa usingizini
Aya za kumsomea Mgonjwa aliyepatwa na jinni wa kutupiwa au jinni wa upepo mbaya(pepo) pia ayah hizi zinaandikwa kama Kombe kwenye karatasi safi na kulowekwa na kupewa mgonjwa kunywa na kujipaka mwilini kwa muda wa masiku ambayo tiba yake itakuwa ianendelea.Tiba hii ni kunywa , kujipaka na kusomewa.Aya hizi pia huweza kutumika kuweka kwenye mafuta ya Zaituni ili mgonjwa awe anajipaka

01.Surat Al-Fatiah 1:1-7
02. Surat Al-Baqarah 2:1-5
03.Surat Al-Baqarah 2:163-164
04. Surat Al-Baqarah 2:255-257
05. Surat Al-Baqarah 2:285-286
06.Surat Al-Imraan 3:18-19
07.Surat Al-A’raaf 7:54-56
08. Surat Al-Muminoon 23:115-118
09.Surat Al-Saffaat 37:1-10
10.Surat Al- Ahqaaf 46:29-32
11. Surat Al-Rahmaan 55:33-36
12. Surat Al-Hashr 59:21-24
13. Surat Al-Jinn 72:1-9
14. Surat Al-Humazah 104
15.Surat Al-Ikhlaas 112
16.Surat Al-Falaq 113
17. Surat An-Nas 114


Kujilinda nafsi yako dhidi ya uchawi na majini kwa kila siku
1.Sema Audhubillah Minashaitwani Rajiim
2.Soma Surat Al-Falaq na Surat An-Naas
3. Soma Ayat Al-Kursiy
4. Soma Surat Al-Baqarah yote
5. Soma vipande vya mwisho vya Surat Al-Baqarah
6.Soma Aya za mwanzo za surat Ghaafir
7.Soma Hizbu al Bahr, Hizbu Barr na Hizbu Nasr za Imam Abal Hassan As-Shadhili
8. Kithirisha kusema maneno haya
Laa ilaaha ill-Allah wahdahu laa shariika lahu, lahu’l-mulk wa lahu’l-hamd wa huwa ‘ala kulli shay’in qadiir

8. Fanya Dhikr muda mwingi na hudhuria daira za Dhikr na Hadhara kwenye misikiti ifanyayo dhikr kwa pamoja
9. Kuwa na udhu wakati wote na kuswali swala zako kwa Jamaa na kwa wakati

Aya za Kuwadhibu majini wa kichawi na majinni wa upepo mbaya(pepo)
01. Surat Al-Fatiah 1:1-7
02.Surat Baqara , Ayat Al-Kurisy 2:255
03.Surat Al-Nisa 4:167-173
04.Surat Al-Maa’idah 5:33-34
05. Surat Al-An’aam 6:93
06. Surat Al-A’raaf 7:44-51, 102-103
07. Surat Al-Anfaal 8:12-13
08. Surat Al-Tawbah 9:7
09. Surat Ibraheem 14:15-17, 42-52
10.Surat Al-Hijr 15:16-18
11.Surat Al-Isra’ 17:110-111
12. Surat Al-Anbiya’ 21:70
13.Surat Al-Dukhaan 44:43-52
14. Surat Al-Ahqaaf 46:29-34
15. SuratAl-Hajj 22:19-22
16.Surat Maryam 19:68-72
17.Surat Al-Mulk 67:5-11
18 Hizbu Bahr na Hizbu Nasr

0 comments:

 
Design by Kwetu Bongo